MTEGO WA SHETANI KWENYE DHAMBI

| Makala

MTEGO WA SHETANI KWENYE DHAMBI:

Bwana Yesu asifiwe sana mpendwa na mshirika wa madhabahu ya siri za biblia,

Naomba niseme na wewe kidogo muda huu kwenye eneo la dhambi,eneo ambalo limekuwa mtego mkubwa sana unaoangusha wengi kwenye wokovu na kuondokewa na uwepo wa Mungu maishani mwao.

Mara zote unapotenda dhambi au uovu fulani,kumbuka kwenye akili yako kuwa yapo mambo makuu mawili yana uhakika mkubwa sana wa kukupata;

Biblia inasema kuwa “Mshahara wa dhambi ni mauti” {Warumi 6:23}, Maana yake kuna kifo cha kiroho na mara nyingi mpaka vifo vya kimwili hujitokeza katika mazingira haya na kuondoa watu kabisa, ili tu wasipate nafasi ya kutubu.

Biblia inasema kuwa “Au waudharau wingi wa wema wake na ustahimili wake na uvumilivu wake,usijue ya kuwa wema wa Mungu wakuvuta upate kutubu? {Warumi 2:4}

USHAURI WANGU KWAKO LEO:

Omba Rehema za Mungu akusamehe na pia hakikisha unapofanya toba kwa habari ya maovu yako, zingatia moyoni mwako kutorudia tena kwa kufuata yafuatayo:

Sababu ni makosa kuanguka dhambini, ila ni makosa makubwa zaidi kunguka palepale ulipoanguka mara ya kwanza, grow spiritually, wasikuangushe angushe tu.

NB:USICHEZE NA DHAMBI, sababu DHAMBI HAINA MCHEZO NA MTU.

Pastor Innocent Mashauri

Madhabahu ya SIRI ZA BIBLIA

Maarifa ya ki-Mungu

+255 758 708 804

Usiongeze ukaribu zaidi na mtu aliyekuangusha dhambini mwanzo {maana ameshakuonyesha kuwa yeye ni nani na kusudi lake ni lipi, muheshimu ila usimpe muda wako zaidi

Usiyazoee tena mazingira yaliyokuangusha mwanzo

Shetani kuweka uzito wa kutubu na kujikuta unaanza taratibu kuizoea dhambi

Shetani kukatisha uhai wako ili usipate nafasi ya kutubu


 SADAKA